Tuesday 27 March 2012



VAZI LA TAIFA



Miongoni mwa mambo ambayo ni ya msingi kwa  Taifa letu na wananchi wake ni kuwa na utambulisho ambao utamfanya kila mwananchi wa  nchi hii atakapoonekana basi atambuliwe kuwa ni Mtanzania.

Miongoni mwa mambo hayo ni vazi la Taifa.

Kumekuwa na mawazo mengi juu ya vazi gain linalofaa kuwa vazi la  Taifa. Mimi nami kama Mtanzania sina budi kuchangia juu ya suala hili.

Nimekuwa nikiyaona mavazi mengi yanayopendekezwa kuwa mavazi ya Taifa. Tatizo nililogundua ni kuwa kwa kiasi Fulani tumekuwa nyuma kiubunifu kiasi kwamba mavazi au mitindo mingi inayoonyeshwa au kupendekezwa ni kama tunairudia au kuiiga toka kwa mataifa mengine.
 
Mimi kwa maoni yangu ningelipenda sisi tujikite katika rangi nne kwanza za taifa ambazo ni kijani; kwamba mtu awe huru kushona mtibndo wowote autakao, lakini pindi utakapokuwa umepangilia rangi zetu zote nne za taifa yaani kijani, njano, bluu na nyeusi basi vazi hilo liwe tayari ni la taifa.
 


Pendekezo langu la pili ni kutumia mavazi ya kimasai lakini katika rangi za taifa, basi hilo nalo liwe vazi la Taifa. Nasema hivi si kwamba ninadharau mavazi ya makabila mengine, lakini tutake tusitake, wamasai ndilo kabila pekee ambalo likekuwa na msimamo wa kulinda vazi lao kila waendako na kila waliko bila ya kuyumbishwa na mavazi haya ambayo yamekuwa yakiingia nchini mwetu kila siku. Hivyo Taifa kwa kuwaenzi, ichukue mavazi yao na kuyafanya ni ya Taifa.

No comments:

Post a Comment