VAZI LA TAIFA
Miongoni
mwa mambo ambayo ni ya msingi kwa Taifa
letu na wananchi wake ni kuwa na utambulisho ambao utamfanya kila mwananchi
wa nchi hii atakapoonekana basi
atambuliwe kuwa ni Mtanzania.
Miongoni
mwa mambo hayo ni vazi la Taifa.
Kumekuwa na
mawazo mengi juu ya vazi gain linalofaa kuwa vazi la Taifa. Mimi nami kama
Mtanzania sina budi kuchangia juu ya suala hili.
Nimekuwa nikiyaona mavazi mengi yanayopendekezwa kuwa
mavazi ya Taifa. Tatizo nililogundua ni kuwa kwa kiasi Fulani tumekuwa nyuma
kiubunifu kiasi kwamba mavazi au mitindo mingi inayoonyeshwa au kupendekezwa ni
kama tunairudia au kuiiga toka kwa mataifa
mengine.
Mimi kwa maoni yangu ningelipenda sisi tujikite katika
rangi nne kwanza za taifa ambazo ni kijani; kwamba mtu awe huru kushona mtibndo
wowote autakao, lakini pindi utakapokuwa umepangilia rangi zetu zote nne za
taifa yaani kijani, njano, bluu na nyeusi basi vazi hilo liwe tayari ni la taifa.
Pendekezo
langu la pili ni kutumia mavazi ya kimasai lakini katika rangi za taifa, basi hilo nalo liwe vazi la
Taifa. Nasema hivi si kwamba ninadharau mavazi ya makabila mengine, lakini
tutake tusitake, wamasai ndilo kabila pekee ambalo likekuwa na msimamo wa
kulinda vazi lao kila waendako na kila waliko bila ya kuyumbishwa na mavazi
haya ambayo yamekuwa yakiingia nchini mwetu kila siku. Hivyo Taifa kwa
kuwaenzi, ichukue mavazi yao na kuyafanya ni ya Taifa.
No comments:
Post a Comment