Friday 23 March 2012


UKIHITAJI KUWA MUWAZI







Kuna watu ambao kwa hakika wanashangaza sana. Watu hawa ni watu ambao wana nafsi dhaifu lakini vichwa vigumu. Watu hawa hawana tofauti na maskini jeuri. Aina hii ya watu ni watata na wakati mwingine husababisha matatizo yasiyo ya lazima kwa kugeukia kushoto wakati wanataka kutazama kulia.
Utamkuta mtu katoka kwao hajala na njaa inamuuma. Anakuta kwa jirani au rafiki yake chakula kipi tayari mezani. Anakaribishwa kwa moyo mmoja, lakini yeye ili pengine asionekane mdoezi na ama kwa sababu zake mwenyewe anasema ahsante kwani si muda mrefu ametoka kula; wakati si kweli. Na mungu humheleleza kwa kupiga muayo mkubwa wa njaa unaotoka moshi mbele ya wenyeji wake.


Mvulana atakuwa amempenda msichana. Badala ya kuwa mkweli ataanza na kumsema pembeni kwa maneno ya kejeri na kashfa nyingi wakati rohoni hajiwezi na yu taabani juu ya msichana huyo.
Yapo mambo mengi makubwa na madogo ambayo huwasibu watu katika uhitaji lakini kwa namna ya ajabu watu hao hujikuta wanapingana na nafsi zao.
Sijaelewa bado, kwanini mtu asiseme ukweli wake kuwa anahitaji badala ya kujivunga  kwa kuwa kisebusebu wakati kiroho kikiwa papo.






No comments:

Post a Comment