Wednesday 21 March 2012



TUMELOGWA KWA FUTIBOLI


Taifa Stars



 Watanzania nadhani tunatakiwa tujiweke sawa kwa ajili ya kazi ya kumtafuta mganga ili atutibu kutokana na ulozi tuliofanyiwa na wazungu na watani zetu wa Afrika ya Magharibi kuwa kusiweze kabisa kucheza futiboli, sisi tuwe ni watu wa mdumange, kiduku, sindimba; labda tukijitahidi sana basi iwe ni raggae ama kwaito.
Lazima tukubali kuwa tumefanywa misukule wa soka kutokana na kuchanganyikiwa kwetu kiasi cha kushindwa tuanze na lipi na lifuatie lipi ili tuweze na sisi kuwa kama wenzetu; japo isiwe kila siku lakini angalau tufike mbali kidogo katika ulimwengu wa kandanda. Yaelekea tumelogwa tuendelee kuwa kichwa cha mwendawazimu daima.
Si siri kuwa tunawajua wakali wa soka wa dunia nzima. Tumeshajua kuwa ili uendelee kisoka unatakiwa ufanye nini. Cha ajabu badala ya kufanya wafanyavyo wenzetu sisi aidha kwa makusudi lakini nadhani ni kwa kulogwa tunafanya kinyume kabisa. Kwetu mpira ni kula na kunywa kwa sana, baada ya kushiba malumbano, matusi, shutuma na mbwembwe.
Nakumbuka siku za nyuma mimi na wenzangu wakeleketwa tulikwenda kwa mganga akatuambia tufanye yafuatayo kama kweli tunataka nchi isinge mbele kimichezo:
1. Tuchague viongozi wapenda soka sio wapenda madaraka kama uncle  kosa ukimchagua anataka abakie hapo milele
2.Tuchague viongozi wanaojua soka sio wanaojua mizengwe
3.Tuchague viongozi wasiokuwa na matumbo(no rushwa and not kwapukwapu)
4.Tuanzishe mashindano ya shule za msingi na sekondari, toka kikata, kiwilaya, kimkoa hadi kitaifa
5.Tuanzishe mashindano ya vyuo, taasisi, wizara n.k. na kwa msisitizo katika majeshi yetu yote hadi zimamoto
6.Tuwe na mashindano ya tarafa, wilaya na mikoa
7.Tuteue shule za michezo kwa kila mkoa na tuwe na vyuo vya michezo japo vitano katika nchi nzima
8.tuwe na chuo kikuu cha michezo tu
9.Tuwe na chuo cha kuzalisha makocha na waamuzi japo kimoja nchini
10.Tuwe na viwanja vya wazi japo viwili kwa miji ya wilaya, vinne kwa miji ya mikoa, na angalau nene kwa miji mikubwa ambako timu mbalimbali zitafanya mazoezi mchana na usiku kutakuwa kukionyeshwa mashindano mbalimbali ya soka duniani bure.
11.TV na redio zetu zirushe matangazo ya mashindano yote ya soka makubwa nchini.
12.Kuwepo na mpango maalum wa kitaifa wa kusambaza vifaa vya michezo mashuleni. Tumwombe Azamu pamoja na kutengeneza juice atengeneze na vifaa vya michezo. Jezi za Azam, mipira ya Azamu na daluga za Azam. Si yeye tu na wenzie akina Azania, Akina Quality Manji na wengineo.
13.Kila mwezi angalau timu mbili za nje zialikwe na TFF kwa ajili ya kuja kuzinoa timu zetu zinazowakilisha nchi. TFF yetu imelala sana tofauti na tunavyotaka iwe.
Baada ya kukamilisha masharti haya tufukie vichwa vya simba, mapembe ya faru na meno ya tembo katika viwanja vyetu vyote ili timu zetu zisifungike pindi zinapocheza nyumbani.
Tukiona mambo bado magumu tukamwome tena ili aangalie wapi tatizo bado lipo.
Lakini toka tutoke kwa mganga huyo tumerudi tumebweteka, kama sio sisi.


No comments:

Post a Comment