UNAPOFIKIA KUJUTIA ASILI YAKO
Hutokea mtu akajuta kimoyomoyo na baadae kujikuta akitamka bayana kuwa anajuta kuwa mwanamume, au anajuta kuwa mhehe, ama anajuta kuwa Mtanzania n.k. Mtu anajikuta anajuta kwa sanabu zake binafsi kiasi cha kuikashfu jamii yake nzima. Mara nyingi hata kile kinachosababisha akajuta huwa kwa ukweli wa mambo hakina msingi. Kujuta wewe kuwa Mtanzania kwa uwingi wake ni kuamini kuwa watanzania wana kasoro.
Unakuta mtu anajuta kuzaliwa mtanzania kwa sababu tu hana kazi au ajira. Anakuwa anawaza kuwa pengine angelizaliwa marekani angelikuwa hana tatizo
Wazo na hisia hizo kidogo zina nafuu lakini inapopindukia na kumkuta mtu anatamka waziwazi tena kwa kujiamini kabisa kuwa ni heri angelizaliwa mbwa uingereza kuliko kuzaliwa mtu
Waswahili wanasema mtu unapokuwa fukara wa mawazo unakuwa unatisha kushinda hata mwendawazimu. Mwanafunzi wa chuo kuona heri angelizaliwa mbwa Ulaya kutokana na kucheleweshewa mkopo, mwanamume kuona heri angelizaliwa mwanamke kutokana na kushindwa kuihudumia familia yake, mwanamke kuona heri angelizaliwa mwanamume kutokana na kunyanyasika kimapenzi n.k. kukurejesha katika mawazo ya kawaida kunahitajika kazi ya ziada.
Mawazo ya aina hii ni matokeo ya watu kujifungia vioo na kujibinafshia matatizo. Kuona wao ndio wenye matatizo makubwa kushinda watu wote. Kutarajia mazuri tu katika maisha
Jamii yetu inahitaji kujiwekea mipango mizuri kimaadili na kitaaluma katika kuhakikisha inajijengea na kujiimarishia uzalendo katika ngazi zote ili vizazi vyetu vipende jamii zao. Jamii zetu zikubali matatizo yaliyopo na ziwe tayari kukabiliana na matatizo hayo. Haitusaidii
Utamaduni wa mtu leo kukosa hela ya bia anakwenda anapita anakashifu serikali, anamkashifu mungu na kila aliyeko mbele yake si utamaduni wa kutufaa. Hata ukijifanya wewe ni msomali,
Hakuna sifa zaidi ya uzalendo. Kujitambua na kujipenda. Jasiri haachi asili. Na ukimsikia mtu anabwata na kujijutia juwa huyo ni maiti anayetembea.
No comments:
Post a Comment