Japo sikutaka lakini naona upo umuhimu wa kulisema hili. Hili ni lawama ya moja kwa moja kwa baadhi ya mama au dada zetu. Wako huru tunakubali, lakini uhuru wao au uhuru wowote hauna budi kuwa na mipaka.
Katika moja ya matumizi mabaya ya uhuru wa akina mama ni vitendo vya kujirahisi na kupendelea kukaa nusu uchi au wengine uchi kabisa mbele ya kadamnasi kwa kisingizio cha usanii, michezo, huduma, ama ngoma.
Ni mara nyingi
Waweza kwenda pia kwenye Hotel ama Bar huko nako kuna vioja vyake. Nadhani watu hawa wanaogopa mkono wa dora vinginevyo wangeliuza vinywaji wakiwa
Wapo wengine utawakuta hawapo Bar wala Disko; pengine madukani, kwenye daladala n.k amevaa nguo ambayo haimruhusu kukaa, kuinama, hata kusimama na kushika chuma kwenye basi. Kila anachokifanya anajikuta kawakalia watu uchi. Ninashindwa kuelewa
Tatizo la macho ni moja, yanapenda kuangalia maasi ama vitu visivyofaa zaidi ya vitu vya kawaida. Sasa ndugu zetu hawa wanapokuwa wamejichanganya katika jamii mara nyingi huwapa wastaarabu wakati mgumu
Kama lengo ni biashara kutokana na soko huria ni vema wangeliomba jiji liwatengee sehemu wafanye biashara
Ebu shangazi zangu wapendwa kaeni mtafakari ni wapi hasa tunakopelekana; vinginevyo mtufafanulie mnapokwenda uchi au kukaa uchi lengo hasa huwa ni nini ? Na je endapo mtaacha kutakuwa na madhara gani na kwa nani ?
No comments:
Post a Comment