GUBU LINAKERA KUPITILIZA
Katika mambo ambayo binadamu wengi hawawezi kuyavumilia; basi ni
gubu.
Mtu mwenye gubu kwa kawaida huwa hana simile, hana subira, hana
shukurani, hana huruma, na nadiriki kusema hata dini hana. Mtu mwenye gubu
hajui kusamehe, hajui kusahau, hajui kubembeleza; yeye daima ni kulaumu,
kulalamika, kusimanga, na kelele kibao. Naweza kusema ni heri ya mkorofi au
mpigaji kuliko mwenye gubu.
Mwenye gubu hana dogo, mwenye gubu haridhiki mwenye gubu daima
mdomo wake uko wazi unamwaga maneno kama bomba
la maji nmachafu.
Mwenye gubu hudhani kuwa yeye ndiye anayejua, yeye ndiye
anayeonewa, yeye ndiye mwangalifu; kwa ujumla mwenye gubu ni mbinafsi. Mwenye
gubu hamwamini mwingine pamoja na kwamba yeye hujion ndiye anaaminika.
Kama hujawahi kuishi na mwenye gubu huwezi kuyajua haya, lakini
kwa wale ambao wamepambana nao wanalijua hili; mwenye gubu ni moto wa kuotea
mbali.
Lakini katika wenye gubu, wapo waliozaliwa na gubu hilo na wapo ambao wanatwezwa na mazingira
au hali ya maisha kwa wakati ule. Pasmoja na tofauti zao hayuko mwenye nafuu.
Niseme tu kuwa gubu linakondesha haraka kushinda hata njaa.
No comments:
Post a Comment