Monday 26 March 2012


ASTE ASTE DADA ZETU…….HUKO TUENDAKO……!




Kwa kipindi cha hivi karibuni nimekuwa nikifuatilia nyenendo za shangazi zangu, dada zangu, shemeji zangu na wengine wakwe zangu; ninachokiona kwa hakika ninaingiwa na hofu.

Lazima niseme nineingiwa na hofu; na si mimi peke yangu; tupo wengi.

Hofu hii imekuwa ikinipata sana hasa upande wa burudani. Kwa sasa imekuwa kama kawaida na pengine kugeuka jadi kwa akina mama kupandwa na mori, mzuka na namna utakavyoita pale ambapo burudani hufika kilele.

Haikatazwi mtu kufurahi au kupagawa, lakini sasa imekuwa inapitiliza. Sasa hivi hata kwenye sherehe ndogo tu ya kipuuzi mtu unaogopa kwenda kwani unaweza ukapambana na vituko mpaka ukashangaa.

Waswahili wanasema kila kitu na mahali pake. Lakini pamoja na msemo huo, mama zangu wamekuwa hawaangazi macho kwanza kabla ya kuanza shughuli zao za kuserebuka. Hawaangazi macho kuhakikisha kama wale wanaowaheshimu wapo ama hawapo. Vijana wamekuwa hawajali kama hapa pana wazee, na wazee nao wamekuwa hawaangazi kuona kama hapa pana watoto. Imekuwa kama fasheni kwenye ngoma kuingizwa mambo ya chumbani. Kuvua nguo imekuwa si jambo la ajabu. Masmbo ya kushikana, kulaliana, kutomasana…..eh!

Dada zangu wangelijaribu kidogo kutafakari kwamba miili ya kiafrika si kama ya wazungu. Mzungu anaweza kwenda hata uchi; kwa mwafrika inakuwa kama mdoli unapita. Lakini mswahili akionyesha kiungo chochote nyeti japo kwa mbali, madhara yake yanakuwa makubwa sana. Hiyo ni kwa kuvaa  bado viuno havijakatwa !

Sina uhakika na hali ya baadae ya mwenendo huu, ndiyo maana nawaombeni mama zangu mtuhurumie aste aste……ama mnataka tusije kwenye ngoma mnazocheza ?

No comments:

Post a Comment