ASTE ASTE DADA ZETU…….HUKO
TUENDAKO……!
Kwa kipindi cha hivi karibuni
nimekuwa nikifuatilia nyenendo za shangazi zangu, dada zangu, shemeji zangu na
wengine wakwe zangu; ninachokiona kwa hakika ninaingiwa na hofu.
Lazima niseme nineingiwa na
hofu; na si mimi peke yangu; tupo wengi.
Hofu hii imekuwa ikinipata sana hasa upande wa
burudani. Kwa sasa imekuwa kama kawaida na
pengine kugeuka jadi kwa akina mama kupandwa na mori, mzuka na namna
utakavyoita pale ambapo burudani hufika kilele.
Haikatazwi mtu kufurahi au
kupagawa, lakini sasa imekuwa inapitiliza. Sasa hivi hata kwenye sherehe ndogo
tu ya kipuuzi mtu unaogopa kwenda kwani unaweza ukapambana na vituko mpaka
ukashangaa.
Waswahili wanasema kila kitu
na mahali pake. Lakini pamoja na msemo huo, mama zangu wamekuwa hawaangazi
macho kwanza kabla ya kuanza shughuli zao za kuserebuka. Hawaangazi macho
kuhakikisha kama wale wanaowaheshimu wapo ama
hawapo. Vijana wamekuwa hawajali kama hapa pana wazee, na wazee nao wamekuwa
hawaangazi kuona kama hapa pana watoto.
Imekuwa kama fasheni kwenye ngoma kuingizwa mambo ya chumbani. Kuvua nguo
imekuwa si jambo la ajabu. Masmbo ya kushikana, kulaliana, kutomasana…..eh!
Dada zangu wangelijaribu
kidogo kutafakari kwamba miili ya kiafrika si kama
ya wazungu. Mzungu anaweza kwenda hata uchi; kwa mwafrika inakuwa kama mdoli unapita. Lakini mswahili akionyesha kiungo
chochote nyeti japo kwa mbali, madhara yake yanakuwa makubwa sana . Hiyo ni kwa kuvaa bado viuno havijakatwa !
Sina uhakika na hali ya
baadae ya mwenendo huu, ndiyo maana nawaombeni mama zangu mtuhurumie aste
aste……ama mnataka tusije kwenye ngoma mnazocheza ?
No comments:
Post a Comment