AJALI
HAINA KINGA
Siku
zote watu tunapokuwa wazima huwa tunajisahau sana . Huwa tunadhani wanaostahili kupata
ajali ni wengine na sisi hatumo katika orodha hiyo; na wakati mwingine huwa
tunafikia hata kukufuru kwa kudhani waliopata ajali walijitakiwa wenyewe ama ni
wajinga.
Moja
ya maeneo ambayo wengi wetu tumebweteka ni katika vyombo vya usafiri. Laiti
kama mungu asingeliingilia kati na kuachia kila uzembe unaofanyika katika
vyombo vya usafiri uzae matunda, basi nadhani kufikia leo zaidi ya nusu ya
wakazi wa dunia hii wangelikuwa wametoweka kwa ajali.
Utamkuta
dareva amejaza abiria kwenye gari lake
anakwenda mwendo ambao hata kama
itatokezea hitilafu yoyote japo ndogo aidha barabarani ama katika gari lake basi
hatakuwa na namna yoyote ya kuokoa maisha ya watu aliowabeba.
Sambamba
na madereva, na abiria nao mara nyingi wanachangia kwani ni wepesi wa kuhimiza
dareva aende mwendo kasi ili waweze kuwahi waendako ama wakati mwingine ni
asili ya ushabiki usio na sababu wa kupenda mwendo mkali.
Zamani
tatizo lilikuwa katika magari, lakini sasa hivi kumekuja usafiri wa pikipiki au bodaboda. Vyombo hivi vimekuwa ni
hatarishi kiasi ambacho tunaweza kusema ni janga la Taifa. Jamaa waendeshao
vyombo hivi wamekuwa wakorofi barabarani kiasi kwamba maisha yao
wamekwisha yakabidhi mbinguni na wao wanatembea
wakiwa kama maiti watembeao. Bodaboda
hawajali kama kuna kuanguka ama kugonga,
wanachokijua wao ni kufika haraka iwezekanavyo huko waendako.
Abiria
wa bodaboda nao sijui ni kwa sababu ya ukata ama vipi, hulazimisha kupanda
wengi katika pikipiki moja kana kwamba wako
katika mchezo wa sarakasi. Wengine kama si wanene hupanda watatu na
dareva kuwa wane katika pikipiki moja; wenyewe wanaita mishikaki.
Sasa
kama tunafanya uzembe wa makusudi kwa kisingizio cha kuwa ajali haina kinga
tuendelee mpaka yaje kutukuta na hapo ndipo tutakuja kujua kama
ajali ina kinga au haina.
No comments:
Post a Comment