MAPENZI HAYALAZIMISHWI
Kuna suala moja muhimu ambalo kwa hakika huwa linaleta usumbusu
mkubwa kwa wanaokutwa nalo. Suala hili huwa ni la kupendwa.
Ukiangalia kwa haraka utaona kuwa kupendwa ni jambo zuri la lenye
neema. Lakini hapo hapo kupendwa katika mgawanyiko wake suala hili hugeuka
kero kwa kuuteka uhuru wa mtu na kuwa adha.
Kupendwa ninakoongelea mimi ni yale mahusiano ya ndani ya jinsia
mbili. Mahusiano haya huwa ni lulu na tunu pale tu ambapo ipo ridhaa ya pande
zote mbili, lakini kinyume cha hapo huwa ni utumwa kwa mmoja anayelazimishwa.
Wapo wakorofi ambao huamini kuwa kwa jinsi walivyo wanaweza
kupendwa na mtu yeyote wakati wowote. Na pindi wanapokuta hali ni kinyume cha
walivyoterajia huanza vita na mapambano ya kutaka kuhakikisha wanapata upendo
walioukusudia.
Utamkuta mwanamke au mwanamume amempenda mtu, bila kutumia
njia za kistaarabu kuyauza mapenzi yake kwa ampendae na kuendesha michakato halali
ya kuteka moyo wa ampendae hukurupuka na kujihesabu kuwa tayari na yeye
anapendwa au atapendwa. Kwa hisia hizo hizo huendesha harakati za mapenzi
wakati huyo apendwaye hana habari, hahitaji, hajisikii na wala hana ndoto
zozote za mahusiano hayo.
Matokeo ya harakati hizi huwa ni visa, manung'uniko, shutuma,
matusi, ugomvi na wakati mwingine husababisha hata vifo kwa aidha aliyependwa
kuuliwa, ama anayependa kujiua ama wote kuuawa.
Ni kweli kuwa kipendacho moyo ndicho dawa, lakini tunatambua
kisichopendwa na moyo ni nini ? Basi tukumbuke pia kuwa kisichopendwa na moyo
ni sumu. Mtu kulazimishwa kutumia kitu usichokitaka ni kama kuabndamishwa na mauti na hasa
pale unapoona kuwa unalazimishwa kukereka kwa furaha ya mtu mmoja. Kama hiyo ni rahisi na inavumilika kwanini
yeye asivumilie akakaa kimya au kutumia pindi anapogundua au kutambua kuwa
anayempenda hana mahitaji nae ?
Kila binadamu ana uhuru wa kuwepo duniani na ana utashi binafsi
katika moyo wake. Ni vema watu wakajifunza kuiheshimu hali hii na kuheshimu
nafsi za wengine. Ile hali ya ubinafsi na kujipendelea bila kujali faraja ya
watu wengine ni ukorofi na haufai kabisa katika jamii. Hayuko mtu ambaye
anaweza kuvumilia penda kitu asichoridhika nacho.
No comments:
Post a Comment