Thursday 12 April 2012




KIFO CHA KANUMBA

KULIA TU HAITOSHI BALI TUJIFUNZE KITU





 Tukumbuke daima kila limpatalo binadamu ni fundisho; fundisho kwake kama yu hai ama fundisho kwa waliobaki hai. Watu kumjadili marehemu Kanumba ama Lulu si kosa, ili mradi iwe ni kwa lengo la kujifunza. Wanapaswa waliobaki au tuliobaki tujue nini cha kupunguza ama nini cha kuongeza katika maisha yetu ili tupate ama yasitukute ya Lulu na Kanumba. Watu huhoji palipo na tukio lisilo la
kawaida na hukaa kimya pale penye tukio lililo la kawaida. Mijadala mingi imeshamiri kutokana na tukio zima la kifo cha Kanumba. Kifo cha Kanumba ni cha aina yake. Mahakama na ifanye kazi yake kwa uwezo wake, lakini na sisi tusizibane midomo katika kulitafakari tukio hili. Ebu fikiria, Lulu binti mdogo wa miaka 19 ak.a. 17 amekwenda kwa mpenzi wake a.k.a. mchumba wake a.k.a. msanii mwenzake. Huko nyumbani kumetokea majibizano a.k.a. ugomvi a.k.a msukumano. Lulu kuona Mpenzi a.k.a Mshkaji kadondoka anatoka na kuondoka; anaacha kisanga kwa ndugu yake. Hasubiri kujua hatma ya hali ya majeruhi ambaye ni kipenzi chake  kama ana hitaji msaada wa kukimbizwa hospitali ama huduma ya kwanza. Pengine alikuwa anawahi daladala, tax, ama anafuata gari aliloacha nje aje ambebe ama alikuwa ana kimbia so ama vyovyote vile. Laiti angelitulia na kuangua kilio pale penye tukio na kujutia mbele ya shemeji yake kwa kueleza ilivyokuwa n.k. maswali na udadisi wa akina yakhe usingelikuwa mkubwa. Yawezekana kwa udogo wa umri wake aliona hivyo ndivyo inafaa; lakini Lulu kama alivyokuwa marehemu Kanumba ni maarufu na watu wanamjua kwa kiasi kikubwa; hivyo wana nafasi ya kumweka katika fungu lolote wanaloona linafaa. Sasa wale wanaojifanya hawayaoni yote haya tuwaweke katika kundi gani....la waungwana, wastaarabu ama ndo walewale ? Pole sana Lulu na Mungu ailaze roho ya marehemu Kanumba mahali pema peponi.... Amen. Lakini ni ukweli usiopingika kuwa kifo hiki kimefundisha wengi mambo mengi.

No comments:

Post a Comment