KIFO
CHA KANUMBA
KULIA TU HAITOSHI BALI
TUJIFUNZE KITU
kawaida na hukaa kimya
pale penye tukio lililo la kawaida. Mijadala mingi imeshamiri kutokana na tukio
zima la kifo cha Kanumba. Kifo cha Kanumba ni cha aina yake. Mahakama na ifanye
kazi yake kwa uwezo wake, lakini na sisi tusizibane midomo katika kulitafakari
tukio hili. Ebu fikiria, Lulu binti mdogo wa miaka 19 ak.a. 17 amekwenda kwa
mpenzi wake a.k.a. mchumba wake a.k.a. msanii mwenzake. Huko nyumbani kumetokea
majibizano a.k.a. ugomvi a.k.a msukumano. Lulu kuona Mpenzi a.k.a Mshkaji
kadondoka anatoka na kuondoka; anaacha kisanga kwa ndugu yake. Hasubiri kujua
hatma ya hali ya majeruhi ambaye ni kipenzi chake kama ana hitaji
msaada wa kukimbizwa hospitali ama huduma ya kwanza. Pengine alikuwa anawahi
daladala, tax, ama anafuata gari aliloacha nje aje ambebe ama alikuwa ana
kimbia so ama vyovyote vile. Laiti angelitulia na kuangua kilio pale penye
tukio na kujutia mbele ya shemeji yake kwa kueleza ilivyokuwa n.k. maswali na
udadisi wa akina yakhe usingelikuwa mkubwa. Yawezekana kwa udogo wa umri wake
aliona hivyo ndivyo inafaa; lakini Lulu kama
alivyokuwa marehemu Kanumba ni maarufu na watu wanamjua kwa kiasi kikubwa;
hivyo wana nafasi ya kumweka katika fungu lolote wanaloona linafaa. Sasa wale
wanaojifanya hawayaoni yote haya tuwaweke katika kundi gani....la waungwana,
wastaarabu ama ndo walewale ? Pole sana
Lulu na Mungu ailaze roho ya marehemu Kanumba mahali pema peponi.... Amen.
Lakini ni ukweli usiopingika kuwa kifo hiki kimefundisha wengi mambo mengi.
No comments:
Post a Comment